NA ROSE MWEKO
MWENYEKITI CCM MKOA WA GEITA APONGEZA UTEUZI WA DKT TULIA AKSON.
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Geita Alhaji Saidi Kalidushi amempogeza Mwenyekiti wa CCM Taifa pamoja na kamati kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa katika mchakato mzima wa kutafuta mgombea wa nafasi ya kiti cha uspika kilicho achwa wazi na aliyekuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyejiuzulu.
Alhaji Kalidushi alisema mchakato wa uchukuaji na urejeshaji wa fomu za kuwania kiti hicho haukuwa mdogo na hivyo ni vyema kupongeza hatua ya kamati kuu kukaa kwa pamoja na kwa kuzingatia sifa za aliyekuwa Naibu spika wa Bunge Dk Tulia Akson ndio ikamteua kuwa mgombea pekee wa kiti hicho nafasi ambayo amekuwa akiifanyia kazi kwa zaidi ya miaka sita sasa.
“tunaipongeza kamati kuu kwa kuchagua mtu ambaye ni mzoefu wa nafasi hiyo kwani kwa muda mrefu ameitumikia hata kama ilikua katika ngazi ya usaidizi lakini kuna kipindi alilazimika kufanya kazi kwa niaba ya aliyekuwa Spika hivyo hiyo nafasi kwake sio ngeni kwamba imeshinde”,
“aidha niwaombe watanzania wenzangu kuachana na mambo ya mitandaoni yanayobeza uteuzi huo kuwa Rais ameanza kuteua wanawake watupu kwakua tu yeye ni mwanamke hii sio sawa kabisa Rais wetu pamoja na kamati kuu inaangalia zaidi sifa za mtu na rekodi ya utendaji kazi wake na sio jinsia Dkt Tulia ni mwanasheria mbobezi na amewahi kushika nafasi mbalimbali n kufanya vizuri aidha ni mzoefu katika bunge hivyo tuungane na kamati kuu kupongeza uteuzi huo kwani naamini utaliletea tija bunge letu tukufu” alisema Alhaji Kalidushi.
Ещё видео!