Kufikia hii leo tume ya IEBC imeweza kuandikisha takriban wapiga kura million 12.7 huku siku ya mwisho ya kujisajili ikiwa ni kesho. Hata hivyo misafara ya idhaa za radio zinazomilikiwa na kampuni ya Royal Media Services iliendelea kupenyeza maeneo mbali mbali kuwarai wale ambao hawajajisajili kutumia fursa hiyo ya mwisho hata mwenyekiti wa RMS DKT S.K Macharia akiungana na baadhi ya misafara hiyo kuonyesha umuhimu wa zoezi hili ambali ni haki yako ya kidemokrasia.
Ещё видео!