Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan leo amekutana na kufanya mazungumzo na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Dkt. Ali Hassan Mwinyi ambaye amempongeza kwa kuanza vizuri majukumu yake ya kuongoza nchi.
Akizungumza baada ya mazungumzo yao, Rais mstaafu Mwinyi amesema amefika nyumbani kwa Rais Samia kumjulia hali, kumtia moyo na kumhakikishia kuwa yeye na Wazee wenzake wapo tayari kutoa ushirikiano na kumsaidia wakati wowote watakapohitajika kufanya hivyo.
![](https://i.ytimg.com/vi/wcaoYpqdSw4/maxresdefault.jpg)