FAHAMU TAFSIRI ZA NDOTO MBALIMBALI.
Ndoto ni eneo ambalo watu wengi wanadanganywa na kupotoshwa Na hiyo yote ni kutokana na kukosa maarifa ya kutosha. Wapo watu wengi mitandaoni, wanaowaeleza watu tafsiri za ndoto mbalimbali zao na mwisho wanaambatanisha na dawa zao za kibishara wakiwadanganya watu kuwa hizo zitaleta suluhisho la matatizo yao.
Wengi wa hao watu kama si wafanyabiashara basi ni waganga wa kienyeji na hawana lolote la kukusaidia zaidi ya kukuongezea matatizo. Kumbuka Ndoto si tatizo la kimwili hivyo hakuna tiba yoyote ya kimwili kama vile dawa ya kunywa au ya kumeza itakayoweza kuleta suluhisho la ndoto zako.
Kwa ufupi Zipo ndoto za aina tatu,
Zinazotokana na Mungu:
Zinazotokana na shetani
Zinazotokana na mtu mwenyewe.
![](https://s2.save4k.ru/pic/xbv2FeZ0Sts/maxresdefault.jpg)