Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda ameiagiza taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU Mkoa wa Arusha kumshikilia Afisa Ardhi wa Halmashauri ya Wilaya ya Arusha Bw. Shevednaze Mwakyokola kwa tuhuma za kushawishi na kupokea rushwa ya Milioni tano suala ambalo Mkuu wa Mkoa amekiri kulishuhudia.
Mkuu wa Mkoa wa Arusha ametoa maagizo hayo leo wakati akizungumza na Wananchi wa Wilaya ya Arumeru kwenye Mkutano wa hadhara leo Mei 28, 2024 kwenye eneo la Ngaramtoni, akisema kuwa aliagiza Mtumishi huyo asimamishwe kazi kupisha uchunguzi na badala yake Mtumishi huyo ameendelea kuwa kazini, akihudhuria pia mkutano huo wa hadhara hii leo.
#sports #entertainment #BONGONEWSTV Usisahau ku-subscribe channel hii kwa taarifa nyingi zaidi na pia tembelea mitandao yetu ya kijamii Instagram @bongonewstz twitter @bongonewstz na Facebook @bongonewstz
![](https://i.ytimg.com/vi/xi0ibf1ymfY/maxresdefault.jpg)