Wakati msimu wa sikukuu za mwisho wa mwaka na mwaka mpya ukiwa umenukia, Kampuni ya usafirishaji ya ABOOD BUS @aboodbustz yenye Makao yake makuu Mkoani Morogoro, leo imetangaza kuanzisha ruti mbili mpya za Mabasi yake ambazo ni kati ya Dar es salaam - Arusha na Dar es salaam - Bukoba.
Taarifa ya Abood kwa Vyombo vya Habari imeeleza kuwa Kampuni hii kongwe iliyoanzishwa mwaka 1986 ikiwa na mabasi zaidi ya 100 kwa sasa, imefanya uwekezaji wa ruti hizi mpya kwa kununua Mabasi mapya ya kisasa aina ya YUTONG ambayo ni 'full luxury' yakiwa na choo ndani, AC, usb chargers, TV na siti za kifahari kwa ajili ya Abiria ku-relax.
"Tunapenda kuwatangazia Watanzania kuwa tumepanua utoaji wa huduma zetu kusafirisha Abiria na mizigo kutoka DSM kwenda Morogoro, Iringa, Mbeya, Tunduma, Mwanza, Tabora na sasa kuna hizo ruti mpya za Dar-Arusha na Dar - Bukoba na mpango wetu ni kwenda Nchi nzima, fanyeni booking kwa kutupigia kama ifuatavyo, wale wa Dar - Arusha 0742999888, wale wa Arusha-Dar 0742999220, wa Dar-Bukoba 0742998008 na wa Bukoba-Dar 0742998018" ——— imeeleza taarifa ya Abood.
![](https://i.ytimg.com/vi/yM9CviO6vKI/mqdefault.jpg)