Mahakama ya Mkoa wa Mwanza imemwachia kwa dhamana aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dk Yahaya Nawanda baada ya kukidhi masharti ya dhamana katika shtaka moja la kulawiti.
Dk Nawanda amepandishwa kizimbani leo Jumanne Julai 9, 2024, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Mkoa wa Mwanza, Erick Marley na kusomewa shtaka hilo na waendesha mashtaka wa Serikali, Magreth Mwaseba na Martha Mtiti.
Mshtakiwa ametimiza masharti hayo na kuachiwa kwa dhamana na shauri hilo limeahirishwa hadi Julai 16, 2024, kwa ajili ya kumsomea mshtakiwa maelezo ya awali na kesi kuanza kusikilizwa.
Endelea kufuatilia Mwananchi
![](https://i.ytimg.com/vi/yMXc3at6hss/maxresdefault.jpg)