Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameagiza kuondolewa kwa madawati yaliyopo katika Shule ya Sekondari ya Iramba Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa ambayo hayana eneo la kuhifadhi madaftari ya wanafunzi.
Agizo hilo amelitoa leo Juni 7,2024 mkoani Iringa wakati akizindua ujenzi wa Shule ya Wasichana Iramba baada ya kubaini kuna madawati ambayo hayana eneo la kuhifadhia madaftari ya wanafunzi.
“Nimeingia darasani nimekuta madawati mmeniambia dawati moja Sh50,000. Madawati ya shule za msingi na sekondari ni lazima yawe na maeneo ya kuweka madaftari ya wanafunzi akikaa juu kuwe na daftari la kuandika ama kitabu,”amesema Majaliwa.
Amesema amejulishwa kila dawati ni Sh50,000 mengine yanayo sehemu ya kuhifadhia na mengine hayana na gharama zilizotumika ni hizohizo haikubaliki.
“Nikitoka hapa leteni lori muondoe haya madawati yote yasiyokuwa na maeneo ya kuhifadhia madaftari yao muyarudishe kwa fundi. Nimesema yarudishwe kwa fundi Mwenyekiti wa Halmashauri simamia hili fedha mmetoa ninyi na usimamizi lazima msimamie.”
Majaliwa amemtaka ofisa elimu kuhakikisha anasimamia jambo hilo, anavyoondoka madawati hayo yaondolewe na kuletwa lenye eneo la kuhifadhi madaftari ya wanafunzi hao.
“Hili ni jambo kubwa ambalo sikuridhika nalo leo ofisa elimu lichukue hilo ni suala lako,”amesema Majaliwa.
#samiasuluhuhassan #simbasc #yangasc #mashabiki #nbcpremeireleague #cafchampionsleague #cafconfiderationcup #ikulumawasiliano #entertainment #music #news #yangasc #simbasc #cafchampionsleague #mayele #highlights #cafconfiderationcup #riversunited #mashabiki #yangaleo #yanga #timuyawananchi #daimambelenyumamwiko #entertainment #music #news #magoliyasimba #magoliyayanga #magoliyote #magoliyamayele #mayele #aziziki #manara #manaraleo #ikulumawasiliano #magufuli #kikwete #mayele #singidabigstars #magoliyamayele #magoliyasimba #magoliyayanga #highlights #azamsportsfederationcup #chama #Shot #mamelodisundowns #alahlytv #alahlysc #miraj
![](https://i.ytimg.com/vi/ymTiFQnexUE/maxresdefault.jpg)