UDHAIFU WA MLANGO WA UZAZI
Udhaifu wa Mlango wa Uzazi ni Hali au shida ambayo huhusisha Mlango wa Uzazi kushindwa kudhibiti au kuzuia Mimba isitoke mpaka kipindi ambacho Mtoto anakuwa amekomaa na tayari kwa ajili ya kuzaliwa au kwa kipindi Cha miezi 9 ya Ujauzito.
Hali hii huchangia asilimia 20 ya Mimba zote zinazoharibika katika Jamii.
Hali au Shida hii kitaalamu huitwa Cervical insufficiency wakati mwingine huitwa Cervical Incompetence.
Udhaifu wa Mlango wa Uzazi au Mlango wa Uzazi kushindwa kuendelea kufunga au kuweza kudhibiti Mtoto asitoke mpaka wakati ambapo Mtoto anakuwa amekomaa vizuri na kuwa tayari kuweza kuzaliwa huweza kupelekea Mjamzito kujifungua mapema zaidi pasipo kuhisi uchungu wowote, hii ni kwa sababu Mlango wa Uzazi huachia pasipo nguvu ya msukumo kutoka kwenye Mji wa Uzazi hususani katika Miezi mitatu ya katikati na Mara baada ya kujifungua Mtoto hufariki.
Je Hali au Tatizo Hilo husababishwa na Mambo gani?.
Tatizo hili au Shida hii Visababishi vyake bado havijajulikana vizuri, japokuwa kitu chochote kile ambacho kinaweza kuhatarisha na kupelekea Mlango wa Uzazi kuwa dhaifu huweza kusababisha tatizo hili na madhara yake huwa ni kuharibika kwa Mimba Mara kwa Mara kutokana na Udhaifu wa Mlango wa Uzazi katika kipindi cha kati cha Ujauzito.
Je ni Mambo gani huweza kuhatarisha kupata Tatizo hili?
Mambo yafuatayo yanaweza kuhatarisha Mwanamke au Mama yoyote kuwa na Tatizo hili la kuwa na Mlango dhaifu usioweza kuhimili Ujauzito mpaka mwishoni mwa Ujauzito, Mambo hayo ni kama;
1. Mwanamke mwenye historia ya kupoteza au kuharibikiwa na Mimba Mara kwa Mara katika kipicha cha Kati cha Ujauzito kati ya wiki 14 hadi wiki 20.
2. Mwanamke mwenye Mlango wa Uzazi mfupi chini ya milimita 25 au sentimita 2.5 ambao umedhibitishwa na kipimo cha Ultrasound inayoingizwa ukeni.
3. Mwanamke mwenye historia yakujifungua Mtoto kabla ya wakati wa kujifungua katika Mimba zilizopita, Mfano kujifungua chini ya wiki 28 za Ujauzito.
4. Mwanamke ambaye Mimba iliharibika na alifanyiwa Upasuaji uliohusisha kutanuliwa kwa Mlango wa Uzazi ili kuweza kusafishwa kutoka na mabaki ya uchafu Mara baada ya Mimba kuharibika.
5. Mwanamke aliyegundulika kuwa ana Udhaifu wa Mlango wa Uzazi katika Mimba zilizopita.
6. Kutolewa au kuondolewa kwa Tishu au kinyama kwa ajili ya utafiti au kama matibabu kwa mama ambae aligundulika ana Saratani ya shingo ya kizazi iliyoko katika hatua za mwanzo.
7. Kuumia au kuchanika kwa Mlango wa Uzazi kipindi ambapo Mama anapojifungua kwa njia ya kawaida au Ukeni ambapo huweza kupelekea Udhaifu wa Mlango wa Uzazi.
8. Upasuaji wa aina yoyote unaohusisha Mlango wa Uzazi huweza kupelekea kupata Udhaifu wa Mlango wa Uzazi.
9. Ulemavu wa Mji wa Uzazi na Mlango wa Uzazi kipindi ambacho Mwanamke apolikuwa anatengenezwa Tumboni mwa mamaye, mfano : Mji wa Uzazi kugawanywa na Kuta moja katikati yake.
10. Kuzaliwa na Udhaifu wa Mlango wa Uzazi endapo mwanamke huyo alizaliwa kutoka kwa Mama aliyekuwa amewahi kumulikwa na mionzi fulani (DES).
11. Kuwa na Mimba ya zaidi ya Mtoto mmoja mfano; Mapacha au Watatu.
Ili kujua Dalili na Matibabu bonyeza link hii sikiliza video
[ Ссылка ]
#DrMwanyika
#MamaAfya
#Vishababishi
#UdhaifuMlangoUzazi
![](https://i.ytimg.com/vi/t3UcziypBWA/maxresdefault.jpg)